Chama cha watanzania nchini Uingereza leo jumamosi ya tarehe 27 mwezi wa tatu kimechagua viongozi wapya watakao kiongoza chama hicho kwa muda wa miaka miwili. Akizungumza kwenye mkutano huo Mwenyekiti mpya wa chama hicho Bw. Lusingu amesema atashirikia na watanzania wote ili kuweza kufanikiwa kukiendelendeleza chama hicho. Katika uchaguzi huo Bw. John Lusingu amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Bi. Nellie Nsemwa amechaguliwa kuwa Mwenyekiti Msaidizi, Bw. Hassan Hafidh amechaguliwa kuwa Katibu, D Makoko amechaguliwa kuwa kuwa Katibu Msaidizi, Bw. Goodluck Mbuya amechaguliwa kuwa Katibu Mwenezi na Dr. Evans Mella amechaguliwa kuwa Mweka Hazina.
Sunday 28 March 2010
TZA yapata viongozi wapya
Posted by Ally Muhdin at 02:48
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment