BLOGGER TEMPLATES - TWITTER BACKGROUNDS »

Welcome - Karibu

Wedding Photography and Video

Monday 23 April 2012

Bank za kiIslam




Bank za kiIslam ni mipangilio mbali mbali na tofauti tofauti ya kibenki kama vile kuhifadhi pesa, kuchukua pesa, kusafirisha pesa kutoka bank kwenda bank nyengine na kutoka nchi moja kwenda nchi nyengine , kufanya biashara kati ya mtu na mtu kwa msaada wa bank, kufanya biashara kati ya mtu kwa kushirikiana na bank, kuuza  bima za kiislam, kutoa mikopo kwa njia za kiislam, Kuuza na kununua hisa kwa utaratibu wa kiislam na mengine mengi. Ni vyema tukakumbushana kwamba bank za kiislam zinatoa huduma kwa waIslam, wasiokua waIslam na hata wale wasiokua na dini yoyote.

 Uhakika ni kwamba bank za kiislam zinakua kwa kasi sana, bado kuna wataalam wachache ktk fani hiyo  na hakuna sehemu nyingi  ambazo watu wanaozungumza Kiswahili wanaweza kupata maelezo mbalimbali kwa lugha yao, tumeona upo umuhimu wa kuanzisha blog maalum ambayo wataweza kupata huduma hizo Kwa kutumia lugha tatu kiSwahili, KiIngereza na kiArabu.

Ni muhimu kukumbushana kwamba mafanikio ya uchumi wowote yanategemea uwiano kati ya maadili na mahitaji ya binadamu, mshikamano wa vitu viwili hivyo ndio ambavyo vinajenga misingi ya uchumi wa kiislam. Kuna wachumi wanaoona kwamba maadili ya uchumi wa kiIslam yanawafanya washirika kugawana hasara na faida kitu ambacho kinasaidia sana kuhamasisha kufanya biashara kwa maslahi ya jamii nzima.

Ukuaji wa bank za kiIslam duniani wenye muelekeo wa kukataa riba ulioanza kujitokeza ktk kipindi takriban cha miaka thalathini iliyopita, umetokana na muelekeo wa kimataifa wa kuzikumbatia banki zinazokubali riba. Kwa mfano sifa kubwa ya mfumo wa uchumi wa banki za kiMagharibi ulitegemea riba kwa kiasi kikubwa sana ambapo ilifikia kiwango hata cha kupuuza dini zao. Kitendo hicho kilizidi kukua kwa kiasi ambacho riba ilikua kama uti wa mgongo ktk uchumi wa Magharibi, kwa upande mwingine uIslam uliendelea kung’ang’ania kwamba riba sio sahihi.

Inatosha kua (Judaism, Christianity, Hinduism na Islam), zenye wafuasi zaidi ya theluthi mbili za watu duniani zimeharamisha Riba. (For the Judaic and Christian views on interest see Johns, et. al., and Noonan (1957) and for the Hindu view, see Bokare (1993), p. 168). Uislamu umeharamisha riba (2:278-279) Pia angalia Biblia, Deuteronomy 23: 19; Leviticus 25:36; Exodus 22:25; Ezekiel 18:5-9. Luke 2:34-35.

Inadaiwa kwamba presha iliyotokana na mfumo  wa bank za kiMagharibi na ombwe lililokuwepo ktk uchumi wa kiIslam, viliwahamasisha wasomi wa kiIslam kujaribu kuulezea uchumi wa kiislam ktk njia za kitaalam zaidi. Wasomi wa kiislam ktk masuala ya kiuchumi waliamua kufuata misingi ambayo ilikubalika ktk dini yao kama vile (Mudarabah), (Muraabaha) ambazo zina maana ya kushirikiana, (Leasing) ambayo ina maana ya kukodisha na aina nyingine nyingi za kiuchumi ambazo zinakubalika kiIslam.

Kwa maelezo zaidi: soma www.ijuebankyakiislam.blogspot.com 

















0 comments:

Search This Blog