BLOGGER TEMPLATES - TWITTER BACKGROUNDS »

Welcome - Karibu

Wedding Photography and Video

Monday 25 February 2013

BALOZI KALLAGHE AKUTANA NA WAFANYABIASHA




Wafanyabiasha Wakitanzania washio jiji la London siku ya Jumamosi, tarehe 23, mwezi 2  walitembelewa na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Peter Kallaghe.


Lengo la ziara hiyo ni kubadilishana nao mawazo na kuangalia jinsi gani wafanyabiashara hao wanavyoweza kutumia fursa za kiuchumi zinazojitokeza nchini Tanzania.

Katika ziara hiyo wafanyabiashara hao walimueleza Balozi Kallaghe mafanikio yao na changamoto zinazowakabili kwanye uendeshaji wa shughuli zao za kila siku.

Wafanyabiashara waliotembelewa ni pamoja na Bi. Jennifer Wright anayemiliki biashara ya kuuza na kununua nyumba pamoja na Soloon za nyele, Bw. Augustino Msey mwenye kampuni ya Swahili Travel and Tours, Moona Store (dukani kwa Sadi) wauzaji wa vifaa vya umeme na wakala wa Westen Union, Salumu wa Barking anayemiliki Foro Barbeque Food, na pia Balozi Kallaghe alipata fursa ya kuhudhuria uzinduzi wa kikundi cha jamii cha Istiqama UK. Balozi Kallaghe aliambatana na wanajumuia ya Kitanzania Bw. Haruna Mbeyu na Bi. Mariamu Mungula.

Balozi Kallaghe alipokutana na mmoja wa wafanyabiashara Bi. Jeniffer Wright alisema kuwa yupo tayari kuwasaidia Watanzania waishio Uingereza na waliokuwepo nyumbani kwa kuwapa mafundisho na maelekezo ya kibiashara kutokana na ujuzi aliokuwa nao. Pia Bi. Wright aliomba serikali ya Tanzania ipunguze vizuizi vya biashara ili waweze kuwekeza nchini Tanzania. Nae Mwenyekiti wa Swahili Group Bw. Augustino Msey alisema kuwa kampuni yake inajitahidi kuitangaza Tanzania katika sekta ya utalii. Bw. Msey aliendelea kusema kuwa kampuni yake inafanya mikakati mikunbwa ya kuwekeza nchini Tanzania. Vilevile Forodhani Barbeque Food waliomba serikali waliangalie suala zima la uraia pacha, kwani Watanzania wanapata tabu sana na vizuizi vingi wanapotaka kuwekeza nchini.

Balozi Kallaghe aliwashauri Watanzania wote wajumuike kwa pamoja, na washirikiane kuleta maendeleo na kuwekeza nchini Tanzania na vilevile wanapopata matatizo wasisite kwenda ubalozini kutaka ushauri na kuomba msaada.

Ally Muhdin - London   


0 comments:

Search This Blog