BLOGGER TEMPLATES - TWITTER BACKGROUNDS »

Welcome - Karibu

Wedding Photography and Video

Wednesday 27 February 2013

ZIARA YA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI MH. SOSPETER MUHONGO NCHINI UINGEREZA


Waziri wa Nishati na Madini Mh. Sospeter Muhongo alipata fursa kuongea na Watanzania waishio Uingereza katika mwaliko rasmi kutoka serikali ya Uingerza. Katika ziara yake nchini Uingereza Mh Sospeter Muhongo ameambata na Bw. Athanas Macheyeki, Bw. Seleman Hatibu na Bw. Sosthenes Massola.

Mh. Muhongo aliwaeleza Watanzani suala zima la gas na jinsi gani serikali itavyotumia gas hiyo kuleta maendeleo ya nchi. Amesema “serikali itahakikisha kuwa kila kijiji kinapata umeme na mpaka kufikia mwaka 2025 nchi ya Tanzania itaondoka na umasikini”. Aliendelea kusema kuwa bila ya umeme hatutoweza kutoa umasikini hivyo wizara yake itatafuta miundo mbinu ya kisasa ili kuwezesha suala zima la matatizo ya umeme linaondoka. Pia amesema wizara yake itaangalia tena ufumo wa Tanesco na kuanzisha idara zingine ambazo zitashirikiana na zitawezesha kutatua matatizo yanayoikabili Tanesco.

Vilevile Mh Muhongo aliwataka wawekezaji wa Kitanzania waweze kuwekeza katika sekta ya nishati na madini.

Habari na Ally Muhdin- London

1 comments:

makala zangu said...

Safi. Ufupisho makini- baada ya hotuba ndefu aliyofanya kwa saa nne bila kupumzika!

Search This Blog