BLOGGER TEMPLATES - TWITTER BACKGROUNDS »

Welcome - Karibu

Wedding Photography and Video

Wednesday 27 March 2013

NAIBU SPIKA WA BUNGE LA TANZANIA MHE JOB NDUGAI AKUTANA NA WATANZANIA WAISHIO UINGEREZA


 Watanzania waishio nchini Uingereza siku ya Jumanne tarehe 27 March walipata fursa ya kukutana na Naibu spika wa Bunge la Tanzania Mheshimiwa Job Ndugai. Katika ziara hiyo Mhe. Ndugai alifuatana na Mhe. Beatrice M Shellukindo, Mhe. Salehe Pamba, Mhe. Godfrey Zambi na Saidi Yakubu.

Watanzania waishio nchi Uingereza walipata kuuliza maswali mbalimbali kuhusu mambo mbalimbali ya maendeleo na kiuchumi yanayoikabili Tanzania kwasababu walishindwa kupata majibu ya maswali hayo kupitia katika vyombo vya habari.

Watanzania hao walitaka kujua hali halisi kuhusu suala la Gesi linaloikabili mkoa wa Mtwara, Elimu, Katiba ya nchi na vyombo vya habari jinsi gani vinavyofanya kazi.

Mhe. Ndugai alisema kuwa serikali inajitahi kuelewesha wananchi wa Mtwara kuhusu suala la Gesi na kutatua migogoro iliyopo baina ya Serikali na wananchi hao. Akongezea kujibu swali hilo Mhe Godfrey Zambi alisema kuwa endapo wananchi wa Kusini wakisema Gesi ni ya kwao peke yao na endapo kila mkoa ukisema unapopata rasimalimali ni yao peke yao tutaweza kujenga nchi? Mhe. Zambi alisema kuwa wananchi wanatakiwa kujua kuwa sisi sote ni wamoja na kila kilichopo na kinachopatika katika mkoa mmoja basi ni cha nchi nzima na si cha mkoa mmoja na kufanya hivyo basi tutaweza kujenga nchi. Mhe. Zambi alisema kuwa serikali itawachukulia hatua viongozi waliohusika kuleta migogoro baina ya wananchi na serikali.

Mheshimiwa Salehe Pamba alijibu suala linakabili vyombo vya habari, alisema kuwa suala hilo serikali inaunda mikakati ili kutatua suala hilo kwani wananchi wengi waishio nchi za nje wamesema kuwa habari wanazozipata si sahihi na ambazo zinaleta utata katika masuala mengi ya kujenga. Watanzania hao walisema kuwa mfano suala la Rais wa China XI Jinping kutembelea nchini Tanzania mara baada ya kuapishwa, vyombo vingi vya habari vimesema Tanzania imeshauzwa, naa kwa kuwa hakuna habari nyingine walizozipata kupitia serikalini Watanzania wengi waishio nje ya nchi waliamini habari hizo ambazo si za kweli. Mhe. Pamba alisema serikali itajadili na kuleta uvumbuzi katika uhuru wa habari na sheria ya kulinda habari nchini Tanzania.

Akijibu suala la katiba Mheshimiwa Beatrice M Shellukindo alisema kuwa Watanzania waishio nje ya nchi wanatakiwa kutoa mawazo katika kuitengeneza katiba mpya ambayo itawasaidia kujenga nchi. Akiongezea kujibu suala la katiba Naibu spika Job Ndugai alisema kuwa katiba yetu haipo sawa na inahitaji marekebisho makubwa. Akitolea mfano nchi ya Kenya alisema kuwa hivi sasa katiba ya Kenya ni nzuri na inawapa mafanikio makubwa katika kujenga nchi yao. Na alitaka Watanzania waige mfano wa katiba ya Kenya ili waweze kuinufaisha nchi yao.

Mhe. Ndugai aliwataka Watanzania wajitokeze kwa wingi katika kutoa mchango wao wa kuchangia katiba kwani kufanya hivyo kutasaidia kujenga nchi yao. Akimalizia aliwashukuru Watanzania waliojitokeza kwenda kukutana na yeye pamoja na msafara wake na amewataka waendelee na msimamo huo endapo watakapokuja viongozi wengine. Kutoka nchini Tanzania. Habari na Ally Muhdin - London


0 comments:

Search This Blog