Viwanja vya ndege vya Aberdeen, Edinbrgh, Glasgow, Belfast and Newcastle vimefungwa kutokana na moshi mkubwa pamoja na mawingu ya kiza yalisababishwa na volcano iliyotanda angani.
Ndege nyingi kutokea viwanja vya ndege vya Heathrow, Gartwick, Stansted, Manchester, Luton and Birmingham zimearisha safari.
Moshi wa Volcano umesababisha uwezekano mdogo wa kuona mbali na hivyo ndege kushindwa kuruka ama kutua katika viwanja vya ndege.
Wasafiri wengi wameathirika na tukio hilo, vilevile wasafiri wote wameshauriwa kupiga simu kujua kama ndege zao zimeaharisha safari kabla ya kwenda kwenye viwanja vya ndege.
0 comments:
Post a Comment