BLOGGER TEMPLATES - TWITTER BACKGROUNDS »

Welcome - Karibu

Wedding Photography and Video

Monday 3 January 2011

Kamanda Ras Makunja kuongoza kikosi kazi jukwaani Serbia

Kamanda Ras Makunja kuongoza kikosi kazi jukwaani Serbia ! Pia Wamepeperusha hewani "Bongo Tambarale"

Bendi machachari ya mzikiwa wa dansi barani ulaya "Ngoma Africa band" aka FFU,wanatarajiwa kutumbuiza katika maonyesho makubwa ya "Kustendorf Film and music festival" yakayo fanyika uko Bergard,nchini Serbia,
Bendi hiyo yenye makao yake nchini ujerumani watatingisha jukwaa la maonyesho hayo siku ya 7-january 2011, maelfu ya washabiki nchini serbia watapelekana puta na mdundo wa "Bongo Dance" kutoka kwao Ngoma Africa band aka FFU,ni mara ya kwanza katika historia ya maonyesho ya mziki nchini Serbia kutumbuizwa na mdundo wa dansi wa kiafrika.

Ngoma Africa Band ni bendi ya mwanzo ya kiafrika kuhalikwa kushiriki katika maonyesho hayo,taarifa ya tovuti ya www.kustendorf-filmandmusicfestival.org unaonyesha jinsi Ngoma Africa band wanavyo utangaza mziki wa Bongo dance la Tanzania katika mataifa !

Kiongozi wa bendi hiyo Ras Makunja aka kamanda ambaye ni mtunzi anayeaminiwa na kutegemewa na jamii...ameibua jipya la mwaka 2011 "Bongo Tambarale" akiimba kwa kushirikiana na Chris-B,ambaye pia mpiga solo gitaa. Bongo Tambarale inatarajiwa kutingisha anga za afrika mashariki na kati wakati wowote.wasikilize ffu www.reverbnation.com/ngomaafricaband www.kustendorf-filmandmusicfestival.org/2011/index.php?p=81

0 comments:

Search This Blog