BLOGGER TEMPLATES - TWITTER BACKGROUNDS »

Welcome - Karibu

Wedding Photography and Video

Thursday, 29 April 2010

Cheryl Cole Achaguliwa kuwa mrembo

Mwimbaji maarufu nchini Uingereza Cheryl Cole ameshika nafasi ya kwanza kati ya warembo maarufu mia moja wa FHM's duniani. Cheryl ameshikilia nafasi hiyo kwa mara ya pili mfululizo sasa.

Mcheza sinema Megan Fox pamoja na Marissa Miller walishindwa kuchukua nafasi hiyo yenye kugombewa na warembo wengi duniani.

Cheryl ambaye ameatengana na mumewe mchezaji wa timu ya Chelsea Ashley Cole, inasemekana kuwa mumewe alifanya mahusiano ya kimapenzi na mwanamke mwingine.

Ijapokuwa alipata matatizo katika ndoa yake lakini aliweza kushika nafasi hiyo ya kwanza na nafasi ya pili kushikiliwa na mcheza tamthilia ya Transformers Megan Fox na nafasi ya tatu kuchukuliwa na mwanamavazi maarufu ya Victoria Secret Merissa Miller.

Mchezaji wa tamthilia ya Twilight Kristen Stewart ameshikilia nafasi ya sita, Kelly Brook ambeye aliwahi kushika nafasi ya kwanza ametokea kuwa katika kumi bora.

Thursday, 22 April 2010

Ryan Air Yakataa Kuwalipa Abiria


Ally Muhdin alipokuwa na Waziri wa mambo ya nje David Milliband.

Ryanair imekataa kuwalipa abria kutokana na matatizo ya usafiri wa anga uliosababishwa na mawingu ya moshi wa Volcano.
Meneja wa shirika la ndege la Ryanair MichaelO'Leary amesisitiza kuwa kampuni hiyo haitahusika na malipo yoyote yaliyosababishwa na mawingu ya moshi wa Volcano.


Ndege hiyo yenye kubana matumizi imesema kuwa haitalipa malipo ya nyumba za kulala wageni pamoja na gharama za chakula.


Bw. O'Leory amesema kuwa abiria wote watarudishiwa gharaza za tiketi na siyo gharama nyingine zozote.


Ryanair kwa siku inabeba abiria wasiopungua 220,000 wa nchi za Ulaya, Lakini Bw. O'Leary amesema hajui abiria wangapi wameathirika na matatizo hayo.


Waziri wa mambo ya Nje nchini Uingereza Bw. David Milliband amesema kuwa mashirika ya ndege yanabidi kuwapa abiria gharama za chakula na makazi ya kulala kwa wale walioathirika na maafa hayo.


Bw. Milliband amesema kuwa itakuwa si kitendo kizuri kama mashirika ya ndege hayatoa huduma hizo.


Wizara yake inajitahidi kuwasaidia raia wate walikumbwa na matatizo ya usafiri vilevile wanajitahidi kuhakikisha shule hazitotoa adhabu kwa wanafunzi wakakao kosa kufanya mitihani kutokana na matatizo ya usafiri.

Tuesday, 20 April 2010

Viwanja Vya Ndege Vyafungwa



Viwanja vya ndege vya Aberdeen, Edinbrgh, Glasgow, Belfast and Newcastle vimefungwa kutokana na moshi mkubwa pamoja na mawingu ya kiza yalisababishwa na volcano iliyotanda angani.

Ndege nyingi kutokea viwanja vya ndege vya Heathrow, Gartwick, Stansted, Manchester, Luton and Birmingham zimearisha safari.

Moshi wa Volcano umesababisha uwezekano mdogo wa kuona mbali na hivyo ndege kushindwa kuruka ama kutua katika viwanja vya ndege.

Wasafiri wengi wameathirika na tukio hilo, vilevile wasafiri wote wameshauriwa kupiga simu kujua kama ndege zao zimeaharisha safari kabla ya kwenda kwenye viwanja vya ndege.

Monday, 19 April 2010


TANGAZO KWA WANA-LONDON

Viongozi wa muda wa Jumuiya ya watanzania London inawaomba watanzania wote waishio London kuhudhuria mkutano wa wana-London utakaofanyika ubalozini siku ya jumamosi tarehe 24-April-10 kuanzia saa 1100 asubuhi. Mkutano huu unategemea kuongelea maswala ya chaguzi wa viongozi na muundo mzima wa jumiya ya London.

Uchaguzi wa viongozi wa London unategemewa kufanyika tarehe 01-May-10. Mawazo yako ni mchango mkubwa kwa jumuiya na kama unazo sifa za uongozi na ari ya kuendeleza jumuiya mlango uko wazi kwa kila mmoja.

Sunday, 18 April 2010

Ubingwa Bado Uko Wazi




King'ang'aniro cha kugombea ubingwa wa ligi nchini Uingereza bado kiko wazi kutokana na matokeo ya michezo ya jana.

Chelsea ambayo inaongoza ligi hiyo iliweza kupoteza mchezo wake muhimu sana ilipofungwa na Tottenham 2-1.

Nayo timu ya Manchester United imeweza kujiweka katika nafasi nzuri katika kutetea taji baada ya kuwafunga majirani zao Manchester City 2-1. Ushindi huo umewawezesha kutofatiana na Chealsea katika kuongoza ligi kwa pointi moja.

Goli pekee la Manchester United lilifungwa katika dakika za nyongeza na kiungo mkongwe Paul Scholes.

Scholes alikuwa peke yake ndani ya kumi na nane na kuweza kufunga goli la kichwa, lililowapa wapenzi na mashabiki wa timu hiyo moyo wa kuchukua ubingwa kwa mara nyingine tena.

Alex Fergurson alifurahi ushindi huo na kusema kwamba timu yake imeweza kufunga magoli dhidi ya Manchester City katika dakika za mwisho mara tatu.


Saturday, 17 April 2010

Elizabeth Taylor Achumbiwa




Dame Elizabeth Taylor ataolewa kwa mara ya nane katika kumbukumbu za maishani mwake.


Habari zinasema kwamba muigizaji huyo maarufu wa tamthilia asiyepungu chini ya umri wa miaka 78 na mpenzi wake wa siku nyingi Jason Winter mwenye umri wa miaka 49 hivi karibuni walikula kiapo cha kuwa pamoja.


Marafiki wa karibu wanasema kuwa "Hakuna kitu cha kuficha wamekuwa pamoja milele na wanapendana... Hivi sasa waimarisha mapenzi yao"


Taylor hivi karibuni alizungumza kwa wazi kuhusiana na jinsi gani anavyompenda Winters, ambaye muda si mrefu tangu awe mkurugenzi wa Janet Jackson's.


Taylor alisema bila kuficha kuwa Jason Winters "Ni mmmoja kati ya wanaume wa ajabu aliowapata kuwajua"

Friday, 16 April 2010

Ashikiliwa na Polisi kwa kosa la Kumtisha Cherly Cole




Kijana mmoja wa kiume alishikiliwa na polisi kwaajili ya uchunguzi kwa kumtupia maneno machafu ya kumtisha Cherly Cole.


Polisi walisema kuwa vitisho na maneno machafu yalitolewa na kijana huyo baada ya kuacha ujumbe kwenye simu ya mkononi ya jaji wa kipindi cha X Factor Dermont O'Leary's mwezi uliopita.


Kijana huyo asiyepungua chini ya umri wa miaka kumi na saba, anatokea Tunbridge Wells, Kent. Alishikiliwa na polisi kwaajili ya kuhojiwa lakini aliachiliwa, Polisi bado wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.


Manchester United yaelekea kupoteza ubingwa

Timu ya Manchester United ambayo inaonekana kuelekea kupoteza ubigwa wa ligi ya Uingereza wana mechi ngumu na majirani zao Manchester City siku ya Jumamosi.


Timu hiyo ambayo hivi karibuni ilitolewa katika king'ang'aniro cha kugombea kombe la mabingwa wa Ulaya, vile vile kupoteza michezo miwili muhimu ya ligi kuu ya Uingereza.Ilifungwa mabao mawili na Chelsea na kutoka sare ya bila bila na Blackburn Rover.

Ukiangalia ligi hiyo ambayo inafikia ukingoni ambapo timu karibia zote zimebakiza mechi nne, Chealse inaonekana kuwa na nafasi kubwa ya kuchukua ubingwa huo japokuwa wana mechi mbili ngumu, Inatakiwa ikacheze Tottenham katika uwanja wa White Hart Lane na Liverpool katika uwanja wa Anfield.

Tegemeo kubwa la timu ya Manchester United, Wayne Rooney ameumia na hiyo ndiyo sababu kubwa ya kushindwa kupata ushindi katika mechi zake za hivi karibuni.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 ameifungia timu yake magoli yasiyozidi 36, na anaoneka kuwa pengo kubwa sana kwa timu hiyo.

Dimitar Berbatov anaonekana bado hajaonesha makali yake, kwani wapenzi wengi wanampinga kutokana na jinsi anavyocheza. Inabidi afanye juhudi za kuweza kuipatia Manchester United magoli yenye kuiwezesha kuchukua ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza.

Wednesday, 14 April 2010

Katie Price Kutoshiriki mbio za Marathon


Mrembo maarufu nchini Uingereza ametangaza kujitoa katika mashindano ya mbio za Marathon. Amefikia uamuzi huo wakutangaza kujiuzulu kupitia tovuti yake lakini hatutamka sababu za ugonjwa ambao unaomfanya aache kukimbia mbio hizo za Marathon.

Uamuzi wa kujito umewafanya watu wawe na tetesi kuwa labda ana mimba ya mtoto wa nne.

Mrembo huyo mwenye umri wa miaka 31 amesema wazi kuwa anajaribu kutafuta mtoto mwingine na mume wake mpya Alex Reid, 34.

Gazeti la OK! limeandika kuwa ameonekana nje ya Hospitali ya Portland huku akiwa ameshikilia tumbo lake.

Price amesema kwenye tovuti yake " Hatoweza kushiriki mbio za Virgin London Marathon kwa mwaka huu."

Aliongezea "nimeweza kufanya mazoezi vizuri na nilikuwa natarajia kukimbia mbio hizo mwaka huu kwaajili ya kuchangisha pesa za chama cha vipofu ( wasioona) lakini doctors wamenishauri nisishiriki mbiyo hizo." Nawatakia kila kila la kheri washiriki wote wa mbio hizo za Marathon.

Reid ambaye alishiriki katika kipindi cha Asubuhi Hii alipoulizwa na mtayarishaji wa kindindi hicho Philip Schofied and Holly Willoughby kama Price ana mimba alijibu kwa kuonyesha na kufunga mdomo wake na kusema "labda inawezekana labda haiwezekani"

Price kama kweli ana mimba basi itakuwa mimba ya mtoto wa nne, tayari anawatoto watatu ambao amezaa na Peter Andre watoto wawili na mmoja amezaa Dwight York.



Tuesday, 13 April 2010

Marehemu Seifu Nassor



Kwaniaba ya familia Alhaji Hussein Nandule napenda kutoa pole kwa familia ya Nassor Bin Jabry kwa kuondokewa na kipenzi chao Marehemu Seif Nassor aliyezikwa leo tarehe 13 mwezi wa April katika makaburi ya kisutu. Marehemu alifariki usiku wa jana. Mola amuweke pahala pema peponi. AMIN

Adebayor ajiuzulu kuchezea timu ya Togo



Mshambuliaji maarufu wa timu ya Manchester City Emmanuel Adebayor ametangaza rasmi kujiuzulu kucheza mechi za kimataifa na kuichezea timu yake ya taifa ya Togo.

Adebayor amechukua uamuzi huo baada ya timu yake ya Togo kushambuliwa walipokuwa katika mashindano ya kombe la Africa nchini Angola.

Timu hiyo ya Togo ilishambuliwa na kusababisha watu watatu kupoteza kufariki.

Akitoa maelezo na sababu za kujiuzulu, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alisema "Kutokana na tukio la shambulizi na ugaidi ambalo limesababisha watu wawili wa nchi mwake kupoteza maisha hiyo ndiyo sababu iliyomfanya kuchukua uamuzi mgumu wa kujiuzulu kucheza mechi za kimataifa"


Akiendelea kutoa maelezo yake alisema kuwa "sisi ni wachezaji mpira tumeenda kucheza mpira na kuiwakilisha nchi yetu, lakini tumevamiwa na watu wanaotaka kupoteza maisha yetu, sitoweza kusahau na sihitaji kutokewa tena na kitendo hicho katika maisha yangu".


Shambulio hilo lilitokea katika mji wa Cabinda nchini Angola. Magaidi waliivamia timu hiyo ya Togo na kuanza kurusha risasi. kitendo hicho kilisababisha mwalimu msaidizi na mwandishi wa timu ya Togo kupoteza maisha, pia dereve wa basi alipoteza maisha. vile vile beki wa timu hiyo Serge Akakpo na mlinda mlango Kodjovi Obilale kuumia. kundi la "The Front for the Liberation of the enclave of Cabinda" linashutumiwa kwa shambulio hilo lakini kundi hilo limekataa kuhusika na shambulio hilo.

Habari na Ally Muhdin, www.tz-one.blogspot.com

Carragher Awajibu wapenzi wa soka



Jamie Carragher amejibu usemi wa wapenzi wengi wa mpira wa miguu ya kuwa Liverpool itapigwa na pengo kubwa itakapokosa kufaulu kucheza mashindano ya mabingwa barani ulaya msimu ujao.


Timu hiyo inayotokea Anfield imeanza kukubaliana na matokea kama kuna uwezekano wa kushindwa kucheza kombe hilo la mabigwa wa ulaya ambolo wameweza kufanikiwa kucheza kombe hilo kwa muda wa miaka saba mfululizo.


Wekundu hao wanashikilia nafasi ya sita katika ligi ya Uingereza baada ya kutoka sare na Fulham siku ya jumapili na wapo pointi sita nyuma ya Manchester City katika kugombea nafasi ya nne, vilevile wamecheza mechi zaidi.

beki huyo wa siku nyingi amesema haoni sababu yoyote kwanini wasiweze kurudi na kuwa na nguvu kubwa zaidi.


'Hakuna kitu kipya kama hatutofanilkiwa, kwani tumeshawahi kucheza na watu wanasahau hivyo' Alisema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32.


'kama hatutofaulu msimu huu ninauhakika msimu ujao hautakuwa mbaya kama msimu huu'.


Carragher aliongezea kwa kusema: 'Tumeuanza msimu vibaya jambo ambalo hatukulitaraji. Tulipenda kushiriki kombe la mabingwa wa ulaya kuliko kombe la ulaya.


Kwa upande wangu kushinda vikombe ndiyo maana ya mashindano na ndiyo mchezo wenyewe, lakini kuna kushindwa pia katika mashindano.


Habari na Ally Muhdin, www.tz-one.blogspot.com



Portsmouth kuomba kibali


nowyherb.png

Portsmouth wanafanya mpango wa kukiomba chama cha mpira nchini Uingereza kiballi cha kucheza kombe la barani ulaya.


Timu hiyo ambayo imeshuka daraja imeweza kujipatia nafasi ya kushirika katika kombe hilo baada ya kuweza kufika fainali za kombe la shirikisho la soka nchi Uingereza ambapo itapambana na Chelsea tarehe 15 May. Timu hiyo iliitoa Tottenham siku ya jumapili.


Portsmouth haitakiwi kushiriki mashindano hayo baada ya kushindwa kuomba kibali hicho, mwisho wa kuomba kibali hicho ulikuwa mwezi wa March 1.


Andrew Andronikou amesema kuwa kuweza kushiriki kwenye mashindano hayo kuleta changamoto kwa wanunuzi wanaotaka kununua timu hiyo. Watafanya kila njia kuweza kufanikisha mashindano hayo kufanyika Fratton Park. kushinda mechi yake


"Nafikiri ni muhimu kuweza kufikilia na kutumia njia zote za kuweza kucheza kombe la Ulaya" Andronikou alisema.


"Inajizungumza yenyewe, itakuwa bora zaidi na mafanikio makubwa kwa timu yetu na kuwavutia wanunuzi wa timu."


Kama watafanikiwa, Portsmouth watachukua nafasi katika ligi ya Ulaya kama washindi wa kikombe cha chama cha mpira nchi Uingereza FA na itaweza kuwaongezea kipato msimu ujao.


Wataki huohuo timu hiyo inataka kuzungumza na timu ya Lens yenye makazi yake nchini Ufaransa kuhusu mchezaji Dindane.


Aruna Dindane mkataba wake ni kuichezea Portsmouth mechi 21, siku ya nusu fainali ndiyo mechi yake ya 21, lakini kama ataendelea kuichezea timu hiyo mechi nyingine itawaghalimu Pompey malipo ya £4


Andronikou anauhakika watafakinikiwa maafikiano na timu hiyo ya Kifaransa.


Habari na Ally Muhdin, www.tz-one.blogspot.com

Sunday, 11 April 2010

Al-HUDAA





Jumuiya ya Al-Hudaa ikishirikiana na New Deal Africa ambayo inaongozwa na Bw. Ayoub Mzee, walifanya sherehe za maulid ya mfungo sita katika ukumbi wa Wally Community Centre, jijini London nchini Uingereza. Maulid hayo yalikuwa kwaajili ya kumkumbuka Mtume Muhammad SWA aliyezaliwa mika 1400 AD iliyopita. Mtume Mohhammad amezaliwa Makka nchini Saudia Arabia, Baba yake ni Abdillah na mama yake Bi. Amina. Waumini na wageni waalikwa toka pande zote za dunia walihudhuria sherehe hizo. Maulid hayo yalijumuisha Dhikri, hotuba mbalimbali na Dua. Kwa taarifa zaidi tembelea www.ayoubmzee.blogspot.com na www.newdealafrica.com. Habari na picha Ally Muhdin

AL-HUDAA



Baadhi ya wageni waalikwa katika Maulid ya Al - Hudaa


Mh.Fadilat Abdul Ramon Jaji aktoa mawaidha

Saturday, 10 April 2010

Amani Awafurahisha Wapenzi wa Muziki jijini London

Baadhi ya wapenzi wa muziki waliojitokeza kuangalia show ya Amani


Mwimbaji maarufu nchi Kenya, Amani kwa mara nyingine tena aliwafurahisha wapenzi wa muziki jijini London. Amani ambaye yupo nchini uingereza kwa ziara mwezi mmoja, alifanya show yake yake tatu katika ukumbi wa Club Africa iliyopo Canning Town, London. Show hiyo ilionekana imefana sana kwani wapenzi wengi walionekana kuridhika na minenguo na kipaji cha uimbaji cha mwanadada huyo. Mwandishi wetu alipowahoji wapenzi wa mwanadada huyo, walisema kuwa sauti ya mwanadada huyo na mashahiri ya nyimbo zake zimefawanya waridhike na tamasha hilo. Vilevile unenguwaji wa mwanadada huyo umewaridhisha sana.

Sunday, 4 April 2010

AMANI AT CLUB AFRIQUE




Saturday, 3 April 2010



Mwimbaji maarufu nchi Kenya, Amani aliwatumbuiza wapenzi wa muziki jijini London siku ya Ijumaa ya tarehe 2 katika ukumbi wa Ambassador, London. Amani atafanya maonyesho manne nchini Uingereza, atatumbuiza Reading, Bristol na London. Mwanadada huyo alianza shughuli zake za muziki miaka saba iliyopita. Beyonce na Mariah carey ndiyo waliomtia changamoto ya kuanzaa kuimba Kenyan Pop. Nyimbo zake nyingi zinahusu mapenzi na anaimba kwa kutumia lugha ya Kiswahili/English. Ameshatoa album moja inayoitwa "Tamani" yenye nyimbo 10. Album hiyo ina nyimbo inayopendwa sana na mashabiki wa muziki "Missing You My Baby". Amani ameshapata tunzo nyingi ikiwemo tunzo ya best female MTV African Awards.



Kutoka Kulia Editor wa BLOG ya TZ-ONE, Ally Muhdin katika Amani na kushoto Dj Richie



Mpiga picha wa BLOG ya TZ-ONE Bw. Shabani Kawawa akiwa na Amani



Bi. Rehema Songambele akiwa na Amani



Imakulata akiwa na Amani, Bi. Imakulata amevutiwa sana na nyimbo za mwanadada huyo.


Promoter DJ Richies akiwa na Amani



Kutoka kushoto DJ Richie, katikati Amani wakibadilishana mawazo muda mfupi kabla ya tamasha kuanza.


DJ Talent akiwa kazini

Search This Blog